Kumbukumbu la Torati 32:34 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 34 Je, sina akiba yake,Muhuri ukiwa umetiwa juu yake katika ghala langu?+ Ayubu 14:17 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 17 Maasi yangu yamefungwa kwa muhuri katika mfuko,+Nawe unatia gundi juu ya kosa langu. Zaburi 90:8 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+ Yeremia 16:17 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 17 Kwa maana macho yangu yako juu ya njia zao zote. Hawakufichwa kutoka mbele zangu, wala kosa lao halikufichwa kutoka mbele za macho yangu.+ Hosea 13:12 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 12 “Kosa la Efraimu limefungwa, dhambi yake imewekwa akiba kama hazina.+ Amosi 8:7 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 7 “Yehova ameapa kwa Ukuu wa Yakobo,+ ‘Kamwe sitazisahau kazi zao zote.+
8 Umeyaweka makosa yetu moja kwa moja mbele zako,+Mambo yetu yaliyofichika mbele za uso wako unaong’aa.+
17 Kwa maana macho yangu yako juu ya njia zao zote. Hawakufichwa kutoka mbele zangu, wala kosa lao halikufichwa kutoka mbele za macho yangu.+