Ayubu
5 Ikiwa siku zake zimeamuliwa,+
Hesabu ya miezi yake iko kwako;
Umeweka amri kwa ajili yake ili asiweze kuvuka.
6 Geuza macho yako kutoka kwake ili apumzike,+
Mpaka apate raha kama mfanyakazi wa kukodiwa anavyopata katika siku yake.
8 Mzizi wake ukizeeka katika udongo
Na kisiki chake kikifa katika mavumbi,
9 Utachipuka unaponusa harufu ya maji+
Nao utatokeza tawi kama mmea mpya.+
12 Mwanadamu pia hulala chini wala haamki.+
Hawataamka mpaka mbingu itakapokuwa haipo tena,+
Wala hawataamshwa katika usingizi wao.+
14 Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?+
Mimi nitangojea siku zote za kazi yangu ya kulazimishwa,+
Mpaka kitulizo changu kije.+
18 Hata hivyo, mlima, unaoanguka, utafifia,
Na hata mwamba utaondolewa mahali pake.
19 Maji kwa hakika yanakula hata mawe;
Kumwagika kwake kunayachukua mavumbi ya dunia.
Ndivyo ulivyoliharibu tumaini la mwanadamu anayeweza kufa.
20 Unamshinda milele hivi kwamba yeye anaenda zake;+
Unauharibu uso wake hivi kwamba unamwacha aende zake.
21 Wanawe hupewa heshima, lakini yeye hajui hilo;+
Nao wanakuwa wasio na maana, lakini yeye hawafikirii.
22 Ila tu nyama yake iliyo juu yake ndiyo itakayoendelea kuuma,
Na nafsi yake ikiwa ingali ndani yake ndiyo itakayoendelea kuomboleza.”