5Nendeni huku na huku katika barabara za Yerusalemu na mwone, sasa, na mjue, nanyi mjitafutie katika viwanja vyake vya watu wote ikiwa mnaweza kumpata mwanadamu,+ ikiwa kuna yeyote anayetenda haki,+ yeyote anayetafuta uaminifu,+ nami nitamsamehe.
2 Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa wasafiri+ katika nyika! Ndipo ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa maana wote ni wazinzi,+ kusanyiko kuu la wanaofanya hila;+
11 Na watu wote wa Israeli wamevunja sheria yako, wamegeuka kando kwa kutotii sauti yako,+ hata ukatumwagia laana na kiapo rasmi+ ambacho kimeandikwa katika sheria ya Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, kwa maana tumemtendea Yeye dhambi.
13 Ole wao,+ kwa maana wamenikimbia!+ Na waporwe, kwa maana wamenikosea! Nami mwenyewe nikachukua hatua ya kuwakomboa,+ bali wao wenyewe wamesema uwongo juu yangu.+