12 Mwishowe Yehoyakini mfalme wa Yuda akatoka kumwendea mfalme wa Babiloni,+ yeye pamoja na mama+ yake na watumishi wake na wakuu wake na maofisa wake wa makao ya mfalme; na mfalme wa Babiloni akamchukua katika mwaka wake wa nane+ wa kuwa mfalme.
6 aliyekuwa amepelekwa uhamishoni+ kutoka Yerusalemu pamoja na watu waliohamishwa ambao walipelekwa uhamishoni pamoja na Yekonia+ mfalme wa Yuda ambaye Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni alimpeleka uhamishoni.
9 Mwishowe wakamweka katika tundu kwa kulabu na kumleta kwa mfalme wa Babiloni.+ Wakamleta kwa kutumia nyavu za kuwindia, ili sauti yake isisikiwe tena katika milima ya Israeli.+