18 “‘Kama ninavyoishi,’ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi,+ ‘kama Tabori+ kati ya milima na kama Karmeli+ kando ya bahari yeye ataingia.
37 “Basi mimi, Nebukadneza, namsifu na kumkweza na kumtukuza Mfalme wa mbinguni,+ kwa sababu kazi zake zote ni kweli na njia zake ni haki,+ na kwa sababu wale wanaotembea kwa kiburi yeye anaweza kuwafedhehesha.”+
14 “Naye amelaaniwa anayetenda kwa ujanja wakati kuna mnyama dume katika kundi lake, naye anaweka nadhiri na kutoa dhabihu ya kilema kwa Yehova.+ Kwa maana mimi ni Mfalme mkuu,”+ Yehova wa majeshi amesema, “na jina langu litakuwa lenye kuogopesha kati ya mataifa.”+