16 Manase pia alimwaga kwa wingi sana damu isiyo na hatia,+ mpaka alipolijaza Yerusalemu kutoka mwisho huu mpaka mwisho ule, mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda dhambi kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ee jiji, linalomwaga damu+ katikati yake mpaka wakati wake ufike,+ na ambalo limefanya sanamu za mavi ndani yake ili kuwa lisilo safi,+
2 Mshikamanifu ameangamia kutoka duniani, na kati ya wanadamu hakuna mnyoofu.+ Wote huvizia ili kumwaga damu.+ Huwinda, kila mmoja ndugu yake mwenyewe, kwa wavu wa kukokota.+
35 ili ije juu yenu damu yote ya uadilifu iliyomwagwa juu ya dunia,+ tangu damu+ ya Abeli+ mwadilifu mpaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, ambaye mlimuua katikati ya patakatifu na madhabahu.+