-
Yeremia 30:10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,” asema Yehova, “wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa wewe kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yao ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi na kuwa huru kutokana na usumbufu naye atastarehe, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayemtetemesha.”+
-
-
Yeremia 44:28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Nao wale wanaookoka upanga, watarudi kutoka katika nchi ya Misri kwenda katika nchi ya Yuda, hesabu yao wakiwa ni wachache;+ na wale wote wa mabaki ya Yuda, wanaoingia katika nchi ya Misri kukaa humo wakiwa wageni, watajua hakika ni neno la nani linalotimia, lile linalotoka kwangu au lile linalotoka kwao.”’”+
-
-
Ezekieli 14:22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Lakini, tazama! jamii iliyoponyoka hakika itabaki ndani yake, wale wanaoletwa.+ Wana na mabinti, tazama! Wanawatokea ninyi, nanyi mtalazimika kuona njia yao na shughuli zao.+ Nanyi hakika mtafarijiwa juu ya msiba ambao nitakuwa nimeuleta juu ya Yerusalemu, naam, yote nitakayokuwa nimeleta juu yake.’ ”
-