-
Isaya 58:13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “Ikiwa kwa ajili ya sabato utarudisha nyuma mguu wako kuhusiana na kuyafanya mapendezi yako mwenyewe katika siku yangu takatifu,+ na kwa kweli uiite sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, inayotukuzwa,+ nawe kwa kweli uitukuze badala ya kufanya njia zako mwenyewe, badala ya kutafuta kinachokupendeza na kusema neno;
-
-
Ezekieli 22:26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 Makuhani wake wenyewe wameitendea jeuri sheria yangu,+ nao wanaendelea kutia unajisi mahali pangu patakatifu.+ Hawatofautishi kati ya kitu kitakatifu na cha kawaida,+ nao hawajafanya chochote kijulikane kati ya kitu kisicho safi na kilicho safi,+ nao wameyaficha macho+ yao yasione sabato zangu, nami ninatiwa unajisi katikati yao.+
-