20 Nami nitautandaza wavu wangu juu yake, naye hakika atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia;+ nami nitamleta Babiloni na kujiweka katika hukumu pamoja naye huko kuhusiana na ukosefu wake wa uaminifu alionitendea.+
8 Na mataifa kuzunguka pande zote kutoka katika wilaya za utawala wakaanza kujipanga dhidi yake+ na kuutandaza wavu wao juu yake.+ Akakamatwa katika shimo lao.+
3 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Pia nitatandaza juu yako wavu+ wangu kwa kutumia kutaniko la vikundi vingi vya watu, nao hakika watakuleta katika wavu wangu wa kukokota.+
5“Sikieni hili, enyi makuhani,+ na mkaze uangalifu, enyi nyumba ya Israeli, na ninyi, enyi nyumba ya mfalme,+ tegeni sikio, kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi; kwa maana mmekuwa mtego+ katika Mispa na kama wavu uliotandazwa juu ya Tabori.+
12 “Njia yoyote ile wanayoiendea, nitatandaza juu yao wavu wangu.+ Nitawashusha chini kama viumbe vinavyoruka vya mbinguni.+ Nitawatia nidhamu kulingana na habari iliyopelekwa kwenye kusanyiko lao.+