29 “Usishangilie,+ Ee Ufilisti,+ yeyote kati yenu, ati kwa sababu fimbo ya yule anayewapiga imevunjwa.+ Kwa maana kutoka katika mzizi wa nyoka+ atatoka nyoka mwenye sumu,+ na tunda lake litakuwa nyoka wa moto anayeruka.+
4 kwa sababu ya siku ambayo inakuja kuwapora Wafilisti+ wote, kumkatilia mbali kutoka Tiro+ na kutoka Sidoni+ kila mwenye kuokoka aliyekuwa akisaidia.+ Kwa maana Yehova anawapora Wafilisti,+ ambao ni mabaki kutoka kisiwa cha Kaftori.+
16 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaunyoosha mkono wangu juu ya Wafilisti,+ nami nitawakatilia mbali Wakerethi+ na kuiangamiza pwani ya bahari inayobaki.+
5 “Ole wao wanaokaa katika eneo la bahari, taifa la Wakerethi!+ Neno la Yehova liko kinyume chenu. Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti, nitakuangamiza wewe pia, hivi kwamba hakutakuwa na mkaaji.+