Sefania
2 Jikusanyeni pamoja, ndiyo, jikusanyeni,+ Ee taifa lisiloona aibu.+ 2 Kabla sheria haijazaa kitu chochote,+ kabla siku hiyo haijapita kama makapi, kabla haijawajilia hasira inayowaka ya Yehova,+ kabla haijawajilia siku ya hasira ya Yehova,+ 3 mtafuteni Yehova,+ ninyi nyote mlio wapole wa dunia,+ ambao mmetenda uamuzi Wake wa hukumu. Utafuteni uadilifu,+ utafuteni upole.+ Huenda+ mkafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.+ 4 Maana Gaza litakuwa jiji lililoachwa;+ na Ashkeloni litakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nalo Ashdodi,+ watalifukuza katikati ya mchana;+ Ekroni nalo litang’olewa.+
5 “Ole wao wanaokaa katika eneo la bahari, taifa la Wakerethi!+ Neno la Yehova liko kinyume chenu. Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti, nitakuangamiza wewe pia, hivi kwamba hakutakuwa na mkaaji.+ 6 Na eneo la bahari litakuwa viwanja vya malisho,+ vyenye visima kwa ajili ya wachungaji na mazizi ya mawe kwa ajili ya kondoo. 7 Nalo litakuwa eneo la mabaki ya nyumba ya Yuda.+ Humo watalisha. Katika nyumba za Ashkeloni, wakati wa jioni, watalala wakiwa wamejinyoosha. Kwa maana Yehova Mungu wao atawakazia fikira zake,+ akusanye na kurudisha walio mateka kati yao.”+
8 “Nimesikia shutuma za Moabu+ na maneno mabaya ya wana wa Amoni,+ ambayo wametumia kuwashutumu watu wangu na kuendelea kujivuna sana juu ya eneo lao. 9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi,”+ asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, “Moabu atakuwa tu kama Sodoma,+ na wana wa Amoni+ kama Gomora, mahali penye upupu, na shimo la chumvi, na mahame yenye ukiwa, mpaka wakati usio na kipimo.+ Mabaki ya watu wangu watawapora, na mabaki ya taifa langu mwenyewe watawamiliki.+ 10 Haya ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+ kwa sababu walishutumu na kuendelea kujivuna sana juu ya watu wa Yehova wa majeshi.+ 11 Yehova atakuwa mwenye kuogopesha juu yao;+ kwa maana ataikondesha miungu yote ya dunia,+ na watu watamwinamia,+ kila mmoja kutoka mahali pake, visiwa vyote vya mataifa.+
12 “Ninyi pia, Waethiopia,+ mtakuwa watu waliouawa kwa upanga wangu.+
13 “Naye atanyoosha mkono wake kuelekea kaskazini, naye ataangamiza Ashuru.+ Naye atafanya Ninawi kuwa mahame yenye ukiwa,+ eneo lisilo na maji kama nyika. 14 Na katikati yake, makundi yatalala yakiwa yamejinyoosha, wanyama-mwitu wote wa taifa.+ Mwari na nungunungu+ watakaa usiku kucha palepale kati ya kombe zake za nguzo.+ Sauti itakuwa inaimba dirishani. Kutakuwa na uharibifu kizingitini; kwa maana atafunua mbao za ukutani.+ 15 Hilo ndilo jiji lenye furaha lililokuwa likikaa kwa usalama,+ ambalo lilikuwa linasema moyoni mwake, ‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine yeyote.’+ Lo! Jinsi amekuwa kitu cha kushangaza, mahali pa wanyama-mwitu kulala wakiwa wamejinyoosha! Kila mtu anayepita kando yake atapiga mluzi; atatikisa mkono wake.”+