4 Na wale wote wa jeshi la mbingu wataoza. Na mbingu zitakunjwa,+ kama vile kitabu cha kukunjwa;+ na jeshi lao lote litanyauka, kama vile majani yanavyonyauka na kuanguka kutoka kwenye mzabibu na kama tini iliyonyauka na kuanguka kutoka kwenye mtini.+
16 Na kutoka Sayuni Yehova atanguruma, kutoka Yerusalemu atatoa sauti yake.+ Na mbingu na dunia zitatikisika;+ bali Yehova atakuwa kimbilio kwa watu wake,+ na ngome kwa wana wa Israeli.+