14 Naye atakuwa kama mahali patakatifu;+ lakini kama jiwe la kujigonga juu yake na kama mwamba wa kujikwaa+ juu yake kwa nyumba zote mbili za Israeli, kama mtego na kama mnaso kwa wakaaji wa Yerusalemu.+
34 Uliendelea kutazama mpaka jiwe likakatwa bila kutumia mikono,+ nalo likaipiga sanamu hiyo juu ya nyayo zake za chuma na za udongo uliofinyangwa, likaziponda.+
44 “Na katika siku za wafalme hao,+ Mungu wa mbinguni+ atausimamisha ufalme+ ambao hautaharibiwa kamwe.+ Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote.+ Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote,+ nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo;+