10 Fimbo ya enzi haitageuka kando kutoka kwa Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo aje;+ na vikundi vya watu vitamtii yeye.+
36 Yesu akajibu:+ “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.+ Kama ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana+ ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu hautoki katika chanzo hiki.”
15 Na malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana+ wetu na wa Kristo+ wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+
6 Mwenye furaha+ na mtakatifu+ ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.+