Mwanzo
49 Baadaye Yakobo akawaita pamoja wanawe, akasema: “Jikusanyeni pamoja niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. 2 Jikusanyeni msikilize, ninyi wana wa Yakobo, ndiyo, msikilizeni Israeli baba yenu.+
3 “Rubeni, wewe ndiwe mzaliwa wangu wa kwanza,+ nguvu zangu na mwanzo wa nguvu zangu za uzazi,+ ubora wa heshima na ubora wa nguvu. 4 Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu,+ kwa sababu umekipanda kitanda cha baba yako.+ Wakati huo ulikinajisi kitanda changu.+ Alikipanda!
5 “Simeoni na Lawi ni ndugu.+ Silaha zao za kuchinjia ni vyombo vya jeuri.+ 6 Ee nafsi yangu, usiingie katika kikundi chao cha rafiki.+ Ee mwelekezo wangu, usiungane na kutaniko lao,+ kwa sababu katika hasira yao waliwaua watu,+ na katika udhalimu wao walikata mishipa ya ng’ombe-dume. 7 Na ilaaniwe hasira yao,+ kwa sababu ni katili,+ na ghadhabu yao, kwa sababu hutenda kwa ukali.+ Acheni niwagawanye katika Yakobo na kuwatawanya katika Israeli.+
8 “Yuda,+ nawe, ndugu zako watakusifu.+ Mkono wako utakuwa katika kikosi cha adui zako.+ Wana wa baba yako watajilaza kifudifudi mbele yako.+ 9 Yuda ni mwana-simba.+ Mwanangu, utapanda kutoka mawindoni. Aliinama, alijinyoosha kama simba, na kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha?+ 10 Fimbo ya enzi haitageuka kando kutoka kwa Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo aje;+ na vikundi vya watu vitamtii yeye.+ 11 Kwa kumfunga punda wake mkomavu kwenye mzabibu na mwana-punda wake mwenyewe kwenye mzabibu mzuri, yeye kwa hakika atafua mavazi yake katika divai na vazi lake katika damu ya zabibu.+ 12 Macho yake ni mekundu kwa divai, na weupe wa meno yake unatokana na maziwa.
13 “Zabuloni atakaa kando ya bahari,+ naye atakuwa kando ya bahari ambapo meli hukaa zikiwa zimetia nanga;+ na sehemu yake ya mbali itakuwa kuelekea Sidoni.+
14 “Isakari+ ni punda mwenye mifupa migumu, aliyelala katikati ya matandiko yenye mifuko miwili. 15 Naye ataona kwamba mahali pa kupumzika ni pazuri na kwamba nchi ni yenye kupendeza; naye atainamisha bega lake abebe mizigo naye atalazimishwa kufanya kazi ya kitumwa.
16 “Dani atawahukumu watu wake akiwa mmoja wa makabila ya Israeli.+ 17 Dani na awe nyoka kando ya barabara, nyoka-bafe kando ya njia, anayeuma visigino vya farasi hivi kwamba mpandaji wake anaanguka nyuma.+ 18 Kwa kweli nitaungoja wokovu kutoka kwako, Ee Yehova.+
19 “Naye Gadi, atavamiwa na kikundi cha waporaji, lakini yeye atavamia upande wa nyuma kabisa.+
20 “Kutoka Asheri mkate wake utakuwa mnono,+ naye atatoa vitu bora vya mfalme.+
21 “Naftali+ ni paa mwembamba. Anatoa maneno ya kupendeza.+
22 “Yosefu ni chipukizi la mti unaozaa matunda,+ chipukizi la mti unaozaa matunda kando ya chemchemi,+ ambao husukuma mbele matawi yake juu ya ukuta.+ 23 Lakini wapiga-mishale waliendelea kumsumbua na kumfyatulia mishale na kuendelea kudumisha uadui kumwelekea.+ 24 Na hata hivyo upinde wake ulikuwa katika mahali pa kudumu,+ na nguvu za mikono yake zilikuwa zenye kunepa.+ Kwa mikono ya Mwenye Nguvu wa Yakobo,+ hapo ndipo alipo Mchungaji, Jiwe la Israeli.+ 25 Yeye ametoka kwa Mungu wa baba yako,+ naye atakusaidia;+ naye yuko pamoja na Mweza-Yote,+ naye atakubariki kwa baraka za mbingu zilizo juu,+ kwa baraka za kilindi cha maji kilicho chini,+ kwa baraka za maziwa na tumbo la uzazi.+ 26 Baraka za baba yako kwa kweli zitakuwa kuu kuliko baraka za milima ya milele,+ kuliko pambo la vilima vinavyodumu mpaka wakati usio na kipimo.+ Zitaendelea kuwa juu ya kichwa cha Yosefu, ndiyo, juu ya utosi wa kichwa cha yule aliyetengwa na ndugu zake.+
27 “Benyamini ataendelea kurarua kama mbwa-mwitu.+ Asubuhi atakula mnyama aliyekamatwa na jioni atagawanya nyara.”+
28 Yote hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno ambayo baba yao aliwaambia alipokuwa akiwabariki. Alimbariki kila mmoja kupatana na baraka yake.+
29 Kisha akawaamuru na kuwaambia: “Mimi ninakusanywa kwa watu wangu.+ Nizikeni pamoja na baba zangu katika pango lililo katika shamba la Efroni Mhiti,+ 30 katika pango lililo katika shamba la Makpela mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, shamba ambalo Abrahamu alinunua kutoka kwa Efroni Mhiti awe na mahali pa kuzikia.+ 31 Huko walimzika Abrahamu na Sara mke wake.+ Huko walimzika Isaka na Rebeka mke wake,+ na huko nilimzika Lea. 32 Shamba lililonunuliwa na pango lililo ndani yake lilitoka kwa wana wa Hethi.”+
33 Basi Yakobo akamaliza kuwapa wanawe amri. Kisha akaiweka miguu yake pamoja juu ya kitanda, akakata pumzi, akakusanywa kwa watu wake.+