Mwanzo
48 Ikawa kwamba baada ya mambo hayo Yosefu akaambiwa: “Tazama, baba yako anadhoofika.” Basi akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu,+ pamoja naye. 2 Kisha Yakobo akaambiwa: “Tazama, mwana wako Yosefu amekuja kwako.” Basi Israeli akajikaza akaketi kitandani mwake. 3 Naye Yakobo akamwambia Yosefu:
“Mungu Mweza-Yote alinitokea Luzi+ katika nchi ya Kanaani apate kunibariki.+ 4 Naye akaniambia, ‘Tazama, nakufanya uzae,+ nami nitakufanya kuwa wengi na nitakufanya uwe kutaniko la vikundi vya watu,+ nami nitaupa uzao wako baada yako nchi hii iwe miliki mpaka wakati usio na kipimo.’+ 5 Na sasa wana wako wawili waliozaliwa katika nchi ya Misri kabla sijaja hapa kwako Misri ni wangu.+ Efraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni.+ 6 Lakini watoto wako utakaozaa baada ya hawa watakuwa wako. Pamoja na majina ya ndugu zao wataitwa katika urithi wao.+ 7 Nami, nilipokuwa nikija kutoka Padani,+ Raheli alikufa+ kando yangu njiani katika nchi ya Kanaani wakati kulipokuwa kungali mwendo mkubwa kabla ya kufika Efrathi,+ basi nikamzika huko kwenye njia ya kwenda Efrathi, yaani, Bethlehemu.”+
8 Kisha Israeli akawaona wana wa Yosefu, akauliza: “Ni nani hawa?”+ 9 Yosefu akamwambia baba yake: “Hawa ndio wanangu ambao Mungu amenipa nikiwa mahali hapa.”+ Basi akasema: “Tafadhali, walete kwangu nipate kuwabariki.”+ 10 Sasa macho ya Israeli yalikuwa yamefifia kutokana na uzee.+ Hakuweza kuona. Basi akawaleta karibu naye, naye akawabusu na kuwakumbatia.+ 11 Na Israeli akamwambia Yosefu: “Sikuwaza ningeuona uso wako,+ lakini tazama, Mungu ameniruhusu nione uzao wako pia.” 12 Kisha Yosefu akawatoa katika magoti yake, naye akainama kifudifudi.+
13 Yosefu akawachukua sasa wote wawili, Efraimu kwa mkono wake wa kuume ukiwa upande wa mkono wa kushoto wa Israeli,+ na Manase kwa mkono wake wa kushoto ukiwa upande wa mkono wa kuume wa Israeli,+ akawaleta karibu naye. 14 Lakini, Israeli akaunyoosha mkono wake wa kuume na kuuweka juu ya kichwa cha Efraimu,+ ingawa ndiye aliyekuwa mdogo,+ nao mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase.+ Aliiweka mikono yake hivyo kwa makusudi, kwa kuwa Manase ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza.+ 15 Naye akambariki Yosefu na kusema:+
“Mungu wa kweli ambaye mbele zake baba zangu Abrahamu na Isaka walitembea,+
Mungu wa kweli ambaye amekuwa akinichunga maisha yangu yote mpaka leo hii,+
16 Malaika ambaye amekuwa akiniponya katika misiba yote,+ awabariki wavulana hawa.+
Na jina langu liitwe juu yao na pia jina la baba zangu, Abrahamu na Isaka,+
Na waongezeke wawe wengi katikati ya dunia.”+
17 Yosefu alipoona kwamba baba yake aliuweka mkono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa,+ naye akajaribu kuushika mkono wa baba yake auondoe juu ya kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.+ 18 Kwa hiyo Yosefu akamwambia baba yake: “Sivyo, baba yangu, kwa sababu huyu ndiye mzaliwa wa kwanza.+ Uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.” 19 Lakini baba yake akaendelea kukataa, akisema: “Najua, mwanangu, najua. Yeye pia atakuwa kikundi cha watu naye pia atakuwa mkuu.+ Lakini, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye,+ nao uzao wake utakuwa hesabu kamili ya mataifa.”+ 20 Naye akaendelea kuwabariki siku hiyo,+ akisema:
“Kupitia kwako Israeli na atangaze baraka tena na tena, akisema,
‘Mungu na akufanye wewe uwe kama Efraimu na kama Manase.’”+
Hivyo akaendelea kumweka Efraimu mbele ya Manase.+
21 Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Tazama, ninakufa,+ lakini Mungu pasipo shaka ataendelea kuwa nanyi na kuwarudisha ninyi katika nchi ya mababu zenu.+ 22 Nami, ninakupa sehemu moja ya nchi zaidi kuliko ndugu zako,+ ambayo niliichukua kutoka katika mkono wa Waamori, kwa upanga wangu na kwa upinde wangu.”