Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 113:1-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 113 Msifuni Yah!+

      Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+

      Lisifuni jina la Yehova.+

       2 Jina la Yehova na libarikiwe+

      Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+

       3 Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+

      Jina la Yehova ni la kusifiwa.+

       4 Yehova amekuwa juu ya mataifa yote;+

      Utukufu wake uko juu ya mbingu.+

       5 Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+

      Yeye anayefanya makao yake juu?+

       6 Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+

       7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+

      Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+

       8 Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+

      Wenye vyeo kati ya watu wake.+

       9 Anampa mwanamke tasa makao katika nyumba+

      Kama mama ya wana aliye na shangwe.+

      Msifuni Yah!+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki