55Haya, ninyi nyote mlio na kiu!+ Njooni kwenye maji.+ Na wale wasio na pesa! Njooni, mnunue mle.+ Ndiyo, njooni, mnunue divai+ na maziwa+ bila pesa na bila bei.+
14 Yule atakayekunywa maji ambayo nitampa hatapatwa na kiu hata kidogo,+ lakini maji ambayo nitampa yatakuwa chemchemi ya maji+ ndani yake, inayobubujika ili kutokeza uzima wa milele.”+
17 Na roho+ na bibi-arusi+ huendelea kusema: “Njoo!” Na yeyote anayesikia na aseme: “Njoo!”+ Na yeyote anayeona kiu aje;+ yeyote anayetaka achukue maji ya uzima bure.+