17 Ndiyo sababu ninamtuma Timotheo kwenu,+ kwa kuwa yeye ni mtoto wangu mpendwa+ na mwaminifu katika Bwana; naye atawakumbusha ninyi njia zangu kuhusiana na Kristo Yesu,+ kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko.
15 Basi, akina ndugu, simameni imara+ na mwendelee kuyashika mapokeo+ mliyofundishwa, iwe kwamba ilikuwa kupitia ujumbe wa maneno au kupitia barua yetu.
6 Sasa tunawapa ninyi maagizo,+ akina ndugu, katika jina la Bwana Yesu Kristo, mjiepushe+ na kila ndugu anayetembea bila utaratibu+ na si kulingana na pokeo mlilopokea kutoka kwetu.+