29 “Mambo yaliyofichwa+ ni ya Yehova Mungu wetu, bali mambo yaliyofunuliwa+ ni yetu na wana wetu mpaka wakati usio na kipimo, ili tupate kuyatimiza maneno yote ya sheria hii.+
17 Yesu akajibu, akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu nyama na damu havikukufunulia hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.+
5 Katika vizazi vingine siri hii+ haikujulishwa kwa wana wa binadamu kama vile ambavyo imefunuliwa+ sasa kwa mitume wake watakatifu na manabii+ kupitia roho,
10 lakini sasa zimefanywa kuwa wazi kabisa kupitia ufunuo+ wa Mwokozi wetu, Kristo Yesu, ambaye amefuta kifo+ lakini ameangaza nuru+ juu ya uzima+ na kutoweza kuharibika+ kupitia habari njema,+
12 Ilifunuliwa kwao kwamba hawakuwa wakijihudumia wenyewe,+ bali walikuwa wakiwahudumia ninyi mambo ambayo sasa mmetangaziwa+ kupitia wale ambao wamewatangazia ninyi habari njema kwa roho takatifu+ iliyotumwa kutoka mbinguni. Malaika wanatamani kuchungulia ndani ya mambo hayo.+