29 Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani,+ na kutahiriwa kwake ni kule kwa moyo+ kupitia roho, wala si kupitia sheria zilizoandikwa.+ Sifa+ ya mtu huyo hutoka, si kwa wanadamu, bali kwa Mungu.+
5 Kwa hiyo msihukumu+ kitu chochote kabla ya wakati unaofaa, mpaka Bwana aje,+ atakayeyaleta kwenye nuru mambo ya siri yaliyo ya giza+ na pia kuyafunua mashauri ya mioyo,+ na ndipo kila mtu atakapopata sifa yake kutoka kwa Mungu.+
15 Fanya kabisa yote unayoweza ili ujitoe kwa Mungu ukiwa mtu aliyekubaliwa,+ mfanyakazi+ asiye na lolote la kuonea aibu,+ ukilitumia sawasawa neno la kweli.+