Waroma
2 Kwa hiyo wewe huna sababu ya kujitetea, Ee mwanadamu,+ hata uwe nani, ukihukumu;+ kwa maana katika jambo lile ambalo unamhukumu mwingine, unajihukumu mwenyewe kuwa una hatia, kwa sababu wewe unayehukumu+ una mazoea ya kufanya mambo hayo hayo.+ 2 Sasa tunajua kwamba, kupatana na kweli,+ hukumu ya Mungu iko juu ya wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo.
3 Lakini je, wewe unafikiri, Ee mwanadamu,+ kwamba utaponyoka hukumu ya Mungu wakati unapohukumu wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo na bado wewe unayafanya?+ 4 Au je, wewe unadharau utajiri wa fadhili+ zake na uvumilivu wenye subira+ na ustahimilivu,+ kwa sababu hujui kwamba sifa ya fadhili za Mungu inajaribu kukuongoza wewe kwenye toba?+ 5 Lakini kulingana na ugumu+ wako na moyo wako usiotubu+ unajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu+ katika siku ya ghadhabu+ na ya kufunuliwa+ kwa hukumu ya uadilifu ya Mungu.+ 6 Naye atamlipa kila mmoja kulingana na matendo yake:+ 7 uzima wa milele kwa wale wanaotafuta utukufu na heshima na kutoharibika,+ kwa uvumilivu katika kazi iliyo njema; 8 hata hivyo, kwa wale wenye ugomvi+ na wale wasioitii kweli+ bali hutii ukosefu wa uadilifu kutakuwa na ghadhabu na hasira,+ 9 dhiki na taabu, juu ya nafsi ya kila mtu anayefanya mabaya, ya Myahudi+ kwanza na pia ya Mgiriki;+ 10 bali utukufu na heshima na amani kwa kila mtu anayefanya mema,+ kwa Myahudi kwanza+ na pia kwa Mgiriki.+ 11 Kwa maana hakuna ubaguzi kwa Mungu.+
12 Kwa mfano, wale wote waliofanya dhambi bila sheria wataangamia pia bila sheria;+ bali wale wote waliofanya dhambi chini ya sheria+ watahukumiwa kwa sheria.+ 13 Kwa maana wasikiaji wa sheria sio walio waadilifu mbele za Mungu, bali watendaji+ wa sheria watatangazwa kuwa waadilifu.+ 14 Kwa maana wakati watu wa mataifa+ wasio na sheria+ wanapofanya kwa asili mambo ya sheria,+ watu hawa, ijapokuwa hawana sheria, wao ni sheria kwao wenyewe. 15 Wao ndio wanaoonyesha kuwa yaliyomo katika sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao,+ huku dhamiri+ yao ikiwatolea ushahidi na, katikati ya fikira zao wenyewe, wanashtakiwa+ au hata kutetewa. 16 Hili litakuwa katika siku Mungu anapohukumu kupitia Kristo Yesu+ mambo ya siri+ ya wanadamu,+ kulingana na habari njema ninayoitangaza.+
17 Sasa, ikiwa wewe ni Myahudi kwa jina+ na unategemea sheria+ na kujivunia Mungu,+ 18 nawe unajua mapenzi yake+ na kuyakubali mambo yaliyo bora kabisa kwa sababu unafundishwa kwa mdomo kutokana na Sheria;+ 19 nawe umesadikishwa kwamba wewe ni kiongozi wa walio vipofu,+ nuru kwa wale walio katika giza,+ 20 mrekebishaji wa wale wasio na akili,+ mwalimu wa watoto wachanga,+ na ukiwa na picha+ ya ujuzi na ya ile kweli+ katika Sheria— 21 hata hivyo, je, wewe unayemfundisha mtu mwingine, hujifundishi mwenyewe?+ Wewe, unayehubiri “Usiibe,”+ je, wewe huiba?+ 22 Wewe, unayesema “Usifanye uzinzi,” je, wewe hufanya uzinzi?+ Wewe, unayechukizwa na sanamu, je, wewe huiba+ katika mahekalu? 23 Wewe, unayejivunia sheria, je, kwa kuivunja Sheria+ unamvunjia Mungu heshima? 24 Kwa maana “jina la Mungu linafanyiwa makufuru katikati ya mataifa kwa sababu yenu”;+ kama ilivyoandikwa.
25 Kwa kweli, kutahiriwa+ kuna faida ikiwa tu unazoea kuifuata sheria;+ lakini ikiwa wewe ni mvunjaji wa sheria,+ kutahiriwa kwako kumekuwa kutotahiriwa.+ 26 Kwa hiyo, ikiwa mtu asiyetahiriwa+ huyashika matakwa+ ya uadilifu ya Sheria, kutotahiriwa kwake kutahesabiwa kuwa kutahiriwa, sivyo?+ 27 Na mtu asiyetahiriwa aliye hivyo kwa asili, kwa kuishika Sheria, atakuhukumu+ wewe ambaye ukiwa na sheria zilizoandikwa na ukiwa na hali ya kutahiriwa unaivunja sheria. 28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye hivyo kwa nje,+ wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje juu ya mwili.+ 29 Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani,+ na kutahiriwa kwake ni kule kwa moyo+ kupitia roho, wala si kupitia sheria zilizoandikwa.+ Sifa+ ya mtu huyo hutoka, si kwa wanadamu, bali kwa Mungu.+