6 Na Yehova Mungu wako atautahiri moyo wako+ na moyo wa uzao wako,+ ili wewe umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote kwa ajili ya uhai wako.+
4 Tahiriweni kwa ajili ya Yehova, na kuondoa magovi ya mioyo yenu,+ ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu; ili ghadhabu yangu isitoke kama moto, na hakika iteketeze bila yeyote wa kuizima, kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu.”+
51 “Ninyi watu wenye shingo ngumu na wasiotahiriwa katika mioyo+ na masikio, sikuzote mnaipinga roho takatifu; kama mababu zenu walivyofanya, ndivyo ninyi mnavyofanya.+
3 Kwa maana sisi ndio wenye tohara ya kweli,+ ambao tunatoa utumishi mtakatifu kwa njia ya roho+ ya Mungu nasi tunajisifu katika Kristo Yesu+ na hatuna uhakika wetu katika mwili,+