24 Kwa maana Makristo wa uwongo+ na manabii wa uwongo+ watatokea na kutoa ishara+ kubwa na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.+
2Hata hivyo, kulikuwa pia na manabii wa uwongo katikati ya wale watu, kama vile pia kutakavyokuwa na walimu wa uwongo katikati yenu.+ Hawa wataingiza ndani kimya-kimya madhehebu yenye kuharibu nao watamkana hata yule bwana aliyewanunua,+ wakijiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
18 Watoto wachanga, ni saa ya mwisho,+ na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi;+ uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho.
2 ‘Mimi nayajua matendo yako,+ na kazi yako ya jasho na uvumilivu, na kwamba huwavumilii watu wabaya, na kwamba uliwajaribu+ wale wanaosema kwamba wao ni mitume,+ lakini wao sio, nawe uliwaona kuwa waongo.