Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 21:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na Shetani akasimama kushindana na Israeli, akamchochea+ Daudi ahesabu Israeli.

  • Ayubu 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na ikaja siku ambapo wana wa Mungu wa kweli+ waliingia na kusimama mbele za Yehova,+ na hata Shetani+ akaingia katikati yao.+

  • Zekaria 3:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kisha malaika+ wa Yehova akamwambia Shetani: “Yehova akukemee,+ Ee Shetani, ndiyo, Yehova akukemee, yeye ambaye analichagua Yerusalemu!+ Je, huyu si kipande cha mti kilichonyakuliwa kutoka motoni?”+

  • Mathayo 4:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake+ ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’ ”+

  • Yohana 13:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Na baada ya hilo tonge ndipo Shetani akaingia ndani ya huyo.+ Kwa hiyo, Yesu akamwambia: “Lile unalofanya lifanye upesi zaidi.”

  • Waroma 16:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwa upande wake, Mungu anayetoa amani+ atamponda Shetani+ chini ya miguu yenu upesi. Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu na ziwe pamoja nanyi.+

  • 2 Wathesalonike 2:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Lakini kuwapo kwa huyo mwasi-sheria ni kulingana na utendaji+ wa Shetani pamoja na kila tendo lenye nguvu na ishara za uwongo na mambo ya ajabu+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki