Zaburi
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.
58 Katika kimya chenu je, kweli mnaweza kusema juu ya uadilifu?+
Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wana wa binadamu?+
2 Badala yake, kwa moyo mnafanya mambo ambayo ni ya kukosa uadilifu kabisa duniani,+
Na kutayarisha barabara kwa ajili ya jeuri ya mikono yenu!+
3 Waovu wamekuwa wapotovu kutoka katika tumbo la uzazi;+
Wametanga-tanga tangu tumboni na kuendelea;
Wanasema uwongo.+
6 Ee Mungu, yang’oe meno yaliyo kinywani mwao.+
Uvunje mifupa ya taya za wana-simba wenye manyoya shingoni, Ee Yehova.
7 Na wayeyuke kana kwamba ni ndani ya maji yanayoenda zake;+
Na aupinde upinde kwa ajili ya mishale yake huku wanapoanguka.+