Zaburi
Kwa kiongozi. “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu. Sauli alipowatuma watu, nao wakaendelea kuilinda nyumba, ili wamuue.+
59 Unikomboe kutoka kwa adui zangu, Ee Mungu wangu;+
Unilinde kutoka kwa wale wanaoinuka dhidi yangu.+
2 Unikomboe kutoka kwa wanaotenda mambo yenye kuumiza,+
Na uniokoe kutoka kwa watu wenye hatia ya damu.
3 Kwa maana, tazama! wamejificha wakiingojea nafsi yangu;+
Wenye nguvu hunishambulia,+
Bila ya uasi wowote upande wangu, wala dhambi yoyote upande wangu, Ee Yehova.+
5 Nawe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ndiye Mungu wa Israeli.+
Uamke uyaelekezee mataifa yote fikira zako.+
Usiwape kibali wasaliti wowote wenye kuumiza.+ Sela.
6 Wao wanaendelea kurudi wakati wa jioni;+
Wanaendelea kubweka kama mbwa+ na kulizunguka jiji pande zote.+
10 Mungu wa fadhili zenye upendo kwangu atanikabili yeye mwenyewe;+
Mungu mwenyewe atanifanya niwatazame adui zangu.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.+
Tumia nguvu zako uwafanye watange-tange huku na huku,+
Na kuwashusha, Ee ngao yetu Yehova,+
12 Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao;+
Na wakamatwe katika kiburi chao,+
Naam, kwa sababu ya laana na udanganyifu ambao wanajizoeza.
Uwakomeshe ili wasiwepo;
Na wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo mpaka kwenye miisho ya dunia.+ Sela.