18 Uhai wake ulipokuwa ukitoka (kwa kuwa alikuwa akifa), akamwita mwana huyo Ben-oni,* lakini baba yake akamwita Benjamini.*+19 Kwa hiyo Raheli akafa na kuzikwa njiani kuelekea Efrathi, yaani, Bethlehemu.+
38 Lakini Yakobo akasema: “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi, kwa sababu ndugu yake amekufa, naye amebaki peke yake.+ Akipatwa na madhara na kufia njiani, basi kwa hakika mtazishusha mvi zangu Kaburini*+ kwa huzuni.”+
7 Wakamjibu: “Mtu huyo alituuliza hivi moja kwa moja kutuhusu sisi na watu wetu wa ukoo: ‘Je, baba yenu angali hai? Je, mna ndugu mwingine?’ nasi tukamwambia ukweli.+ Tungejuaje atasema, ‘Mleteni ndugu yenu huku chini’?”+