Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 3:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Kwa jasho la uso wako utakula chakula* mpaka utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitolewa humo.+ Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.”+

  • Zaburi 146:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Roho* yake hutoka, naye hurudi ardhini;+

      Siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.+

  • Mhubiri 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa maana walio hai wanajua* kwamba watakufa,+ lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe,+ wala hawana thawabu* tena, kwa sababu kumbukumbu lote kuwahusu limesahauliwa.+

  • Mhubiri 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Jambo lolote unalofanya kwa mkono wako, lifanye kwa nguvu zako zote, kwa sababu hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima Kaburini,*+ mahali unapokwenda.

  • Ezekieli 18:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Tazama! Nafsi zote—ni zangu.* Kama nafsi ya baba ilivyo yangu ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu. Nafsi* inayotenda dhambi ndiyo itakayokufa.*

  • Waroma 5:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Hiyo ndiyo sababu, kama vile kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi,+ basi kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi+—.

  • 1 Wakorintho 15:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,+ vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki