26 “‘Siku ya mavuno ya kwanza yaliyokomaa,+ mnapomtolea Yehova nafaka iliyotoka kuvunwa+ katika sherehe yenu ya majuma,+ mnapaswa kuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+
9 “Mtahesabu majuma saba. Mnapaswa kuanza kuhesabu majuma saba wakati mnapoanza kuvuna kwa mundu nafaka iliyo shambani.+10 Kisha mtafanya Sherehe ya Majuma kwa Yehova Mungu wenu+ kwa toleo la hiari linalotoka mkononi mwenu, kulingana na baraka ambazo Yehova Mungu wenu amewapa.+