2“‘Sasa ikiwa mtu atamtolea Yehova toleo la nafaka,+ ni lazima toleo lake liwe la unga laini, naye anapaswa kumimina mafuta juu yake na kuweka ubani juu yake.+
11 “‘Toleo lolote la nafaka mnalomtolea Yehova halipaswi kutiwa chachu,+ kwa maana hampaswi kuuteketeza unga wowote uliokandwa ulio na chachu au kuiteketeza asali ili ifuke moshi ikiwa toleo la Yehova linalochomwa kwa moto.
13 “‘Kila toleo la nafaka mnalotoa linapaswa kukolezwa kwa chumvi; na msiruhusu kamwe chumvi ya agano la Mungu wenu ikosekane katika toleo lenu la nafaka. Kila toleo mtakalotoa, mtalitoa pamoja na chumvi.+