Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 8:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Hata hivyo, makuhani wachawi wakafanya jambo hilohilo kwa mazingaombwe yao, nao pia wakafanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.+

  • Kumbukumbu la Torati 18:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Asipatikane miongoni mwenu mtu yeyote anayemteketeza* motoni+ mwanawe au binti yake, mtu yeyote anayefanya uaguzi,*+ mtu yeyote anayefanya uchawi,+ mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri,+ mlozi,+ 11 mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho,+ mpiga ramli,+ au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu.+ 12 Kwa maana mtu yeyote anayefanya mambo haya ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea haya yanayochukiza, Yehova Mungu wenu anayafukuza mataifa hayo kutoka mbele yenu.

  • Wagalatia 5:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Sasa matendo ya mwili huonekana wazi, nayo ni uasherati,*+ uchafu, mwenendo mpotovu,*+ 20 ibada ya sanamu, kuwasiliana na roho,*+ chuki, mizozo, wivu, milipuko ya hasira, migogoro, migawanyiko, madhehebu,

  • Ufunuo 21:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Lakini kuhusu waoga na wale wasio na imani+ na wale wenye kuchukiza katika uchafu wao na wauaji+ na waasherati*+ na wale wanaozoea kuwasiliana na roho na wanaoabudu sanamu na waongo wote,+ fungu lao litakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti.+ Hili linamaanisha kifo cha pili.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki