30 Siku iliyofuata, Musa akawaambia watu: “Mlitenda dhambi kubwa sana, na sasa nitapanda kwenda kwa Yehova ili nione ikiwa ninaweza kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi yenu.”+
17 “Hakuna mtu mwingine yeyote anayepaswa kuwa ndani ya hema la mkutano kuanzia wakati Haruni anapoingia mahali patakatifu kutoa dhabihu ya kufunika dhambi, mpaka anapotoka nje. Atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe na za nyumba yake+ na za kusanyiko lote la Waisraeli.+
25 Kuhani atatoa dhabihu ya kufunika dhambi ya kusanyiko lote la Waisraeli, nao watasamehewa,+ kwa sababu lilikuwa kosa, nao walimletea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto na kuleta dhabihu yao ya dhambi mbele za Yehova kwa ajili ya kosa lao.
7 Kupitia kwake tunaachiliwa huru kwa njia ya fidia kupitia damu ya huyo,+ ndiyo, msamaha wa makosa yetu,+ kulingana na utajiri wa fadhili zake zisizostahiliwa.
17 Kwa hiyo alipaswa kuwa kama “ndugu” zake katika mambo yote,+ ili awe kuhani mkuu mwenye rehema na mwaminifu katika mambo yanayohusiana na Mungu, ili atoe dhabihu ya upatanisho*+ kwa ajili ya dhambi za watu.+