Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 28:26-31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “‘Siku ya mavuno ya kwanza yaliyokomaa,+ mnapomtolea Yehova nafaka iliyotoka kuvunwa+ katika sherehe yenu ya majuma,+ mnapaswa kuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ 27 Mtatoa ng’ombe dume wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova,+ 28 pamoja na toleo la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya kila ng’ombe dume, na sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume mmoja, 29 sehemu moja ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 30 na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya kufunika dhambi zenu.+ 31 Mtatoa vitu hivyo pamoja na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la nafaka. Mtatoa wanyama wasio na kasoro,+ pamoja na matoleo yao ya kinywaji.

  • Kumbukumbu la Torati 16:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “Mara tatu kwa mwaka, wanaume wenu wote wanapaswa kwenda mbele za Yehova Mungu wenu mahali atakapochagua: katika Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu,+ Sherehe ya Majuma,+ na Sherehe ya Vibanda,*+ na hakuna yeyote kati yao anayepaswa kwenda mbele za Yehova mikono mitupu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki