Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Nanyi mtakuwa kitu cha kutisha na cha kudharauliwa,* na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa mataifa yote ambako Yehova atawapeleka.+

  • Kumbukumbu la Torati 29:22-24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Kizazi cha wakati ujao cha wana wenu na pia wageni kutoka nchi ya mbali watakapoona mapigo ya nchi, magonjwa ambayo Yehova ameleta juu yake— 23 kiberiti na chumvi na kuteketea, hivi kwamba nchi yote haitapandwa wala kuchipuza mimea, wala hakuna mmea wowote utakaoota ndani yake, kama ilivyokuwa wakati wa maangamizi ya Sodoma na Gomora,+ Adma na Seboiimu,+ majiji ambayo Yehova aliyaangamiza katika hasira yake na katika ghadhabu yake— 24 wao pamoja na mataifa yote watauliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii?+ Ni nini kilichomfanya awake hasira kali hivi?’

  • Yeremia 18:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kutisha+

      Na kitu cha kupigiwa mluzi milele.+

      Kila mtu atakayepita kando yake atatazama kwa mshtuko na kutikisa kichwa chake.+

  • Maombolezo 2:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Wote wanaopita barabarani wanakupigia makofi kwa dharau.+

      Wanapiga mluzi kwa mshangao+ na kumtikisia vichwa vyao binti ya Yerusalemu, wakisema:

      “Je, hili ndilo jiji walilosema hivi kulihusu: ‘Lina urembo mkamilifu, ni shangwe ya dunia yote’?”+

  • Ezekieli 5:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Utakuwa kitu cha kushutumiwa na kudharauliwa,+ mfano wa kuonya na tisho kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapotekeleza hukumu dhidi yako kwa hasira na ghadhabu na kwa adhabu kali. Mimi, Yehova, nimesema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki