-
Kumbukumbu la Torati 1:34-38Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 “Wakati huo wote Yehova alisikia mambo mliyokuwa mkisema, akakasirika na kuapa hivi:+ 35 ‘Hakuna mtu hata mmoja wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kwamba nitawapa baba zenu,+ 36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wanawe nchi hiyo aliyoikanyaga kwa miguu yake, kwa sababu amenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.*+ 37 (Yehova alinikasirikia mimi pia kwa sababu yenu, akasema, “Wewe pia hutaingia humo.+ 38 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wako,*+ ndiye atakayeingia katika nchi hiyo.+ Mwimarishe,*+ kwa maana atawawezesha Waisraeli kuirithi nchi hiyo.”)
-