Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 14:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwamba mtaishi ndani yake,+ isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+

  • Hesabu 26:65
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 65 Kwa maana Yehova alikuwa amesema hivi kuwahusu: “Ni lazima wafe nyikani.”+ Kwa hiyo hakuna mwanamume hata mmoja kati yao aliyebaki isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+

  • Hesabu 32:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 ‘Wanaume waliotoka Misri wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi hawataiona nchi+ ambayo niliapa kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote— 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune, Mkenizi, na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.’+

  • Kumbukumbu la Torati 1:35, 36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 ‘Hakuna mtu hata mmoja wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kwamba nitawapa baba zenu,+ 36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wanawe nchi hiyo aliyoikanyaga kwa miguu yake, kwa sababu amenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.*+

  • Yoshua 14:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ndipo watu wa kabila la Yuda wakaenda kwa Yoshua kule Gilgali,+ na Kalebu+ mwana wa Yefune Mkenizi akamwambia: “Unajua vizuri maneno ambayo Yehova alimwambia Musa+ mtumishi wa Mungu wa kweli+ juu yangu na juu yako kule Kadesh-barnea.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki