-
Waebrania 9:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Hema hili ni mfano kwa ajili ya wakati huu,+ na kulingana na mpango huu, zawadi na dhabihu zinatolewa.+ Hata hivyo, haziwezi kufanya dhamiri ya mtu anayefanya utumishi mtakatifu iwe kamilifu.+ 10 Zinahusu vyakula na vinywaji tu na njia mbalimbali za kujisafisha kisherehe.*+ Hayo yalikuwa matakwa ya kisheria kuhusu mwili+ nayo yalifuatwa mpaka wakati uliowekwa wa kunyoosha mambo.
-
-
Waebrania 9:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kwa maana ikiwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe dume+ na majivu ya ndama jike yaliyonyunyizwa juu ya wale ambao wametiwa unajisi hutakasa ili kuusafisha mwili,+ 14 je, damu ya Kristo,+ ambaye kupitia roho inayodumu milele alijitoa mwenyewe kwa Mungu bila dosari, haitazisafisha hata zaidi dhamiri zetu kutoka katika matendo yaliyokufa+ ili tumtolee utumishi mtakatifu Mungu aliye hai?+
-