-
Kutoka 19:19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Sauti ya pembe ilipozidi kuongezeka zaidi na zaidi, Musa akaongea, na sauti ya Mungu wa kweli ikamjibu.
-
-
Kumbukumbu la Torati 4:10-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Siku ambayo mlisimama mbele za Yehova Mungu wenu kule Horebu, Yehova aliniambia, ‘Wakusanye watu mbele zangu ili niwafanye wasikie maneno yangu,+ ili wajifunze kuniogopa+ siku zote ambazo watakuwa hai juu ya ardhi na ili wawafundishe wana wao.’+
11 “Basi mlikaribia na kusimama chini ya mlima, na mlima huo ulikuwa ukiwaka moto uliofika mpaka mbinguni; kulikuwa na giza, wingu, na utusitusi mzito.+ 12 Yehova akaanza kuzungumza nanyi kutoka katika moto.+ Mlisikia maneno, lakini hamkuona umbo lolote+—kulikuwa na sauti tu.+ 13 Naye akawatangazia agano lake,+ alilowaamuru mshike—zile Amri Kumi.*+ Kisha akaziandika kwenye mabamba mawili ya mawe.+
-