Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 13:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Nitakasie* kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Waisraeli. Mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mwanadamu na mnyama ni wangu.”+

  • Kutoka 22:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Hivi ndivyo utakavyofanya kuhusu ng’ombe dume wako na kondoo wako:+ Atakaa na mama yake kwa siku saba. Siku ya nane, utanipa mimi.+

  • Hesabu 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Siku niliyomuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mpaka wa mnyama.+ Watakuwa wangu. Mimi ni Yehova.”

  • Hesabu 18:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Kila mzaliwa wa kwanza wa viumbe wote walio hai,+ ambaye watanitolea mimi Yehova, awe ni mwanadamu au mnyama, anapaswa kuwa wako. Hata hivyo, ni lazima uwakomboe wazaliwa wa kwanza wa wanadamu,+ na unapaswa pia kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.+

  • Hesabu 18:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini hupaswi kumkomboa+ ng’ombe dume ambaye ni mzaliwa wa kwanza au mwanakondoo dume ambaye ni mzaliwa wa kwanza au mbuzi ambaye ni mzaliwa wa kwanza. Hao ni watakatifu. Unapaswa kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu,+ na mafuta yao unapaswa kuyateketeza ili yafuke moshi yakiwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki