36 Kutoka Egloni, Yoshua na Waisraeli wote wakaenda Hebroni+ na kulishambulia. 37 Wakaliteka na kuliangamiza kwa upanga jiji hilo, mfalme wake, miji yake, na wakaaji wote, na hakuna yeyote aliyebaki. Yoshua aliliangamiza pamoja na wakaaji wote, kama alivyofanya kule Egloni.