-
1 Wafalme 2:29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Kisha Mfalme Sulemani akaambiwa hivi: “Yoabu amekimbilia katika hema la Yehova, na yuko humo kando ya madhabahu.” Kwa hiyo Sulemani akamtuma Benaya mwana wa Yehoyada, akisema: “Nenda ukamuue!”
-
-
1 Mambo ya Nyakati 27:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Msimamizi wa kikundi cha tatu kilichopewa zamu ya kutumikia katika mwezi wa tatu alikuwa Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mkuu wa makuhani, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 6 Huyo Benaya alikuwa shujaa hodari miongoni mwa wale 30 na ndiye aliyekuwa msimamizi wao, na kiongozi wa kikundi chake alikuwa Amizabadi mwanawe.
-