-
1 Wafalme 2:31-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Kisha mfalme akamwambia: “Fanya kama alivyosema; muue na umzike, uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu damu ambayo Yoabu alimwaga kwa njia isiyo ya haki.+ 32 Yehova atamlipiza kwa sababu ya damu aliyomwaga,* kwa sababu bila Daudi baba yangu kujua, aliwapiga na kuwaua kwa upanga wanaume wawili walio waadilifu na bora kuliko yeye, yaani, Abneri+ mwana wa Neri mkuu wa jeshi la Israeli,+ na Amasa+ mwana wa Yetheri, mkuu wa jeshi la Yuda.+ 33 Hatia ya damu yao itakuwa juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya kichwa cha uzao* wake milele;+ lakini amani kutoka kwa Yehova na iwe milele juu ya Daudi, uzao* wake, nyumba yake, na kiti chake cha ufalme.” 34 Kisha Benaya mwana wa Yehoyada akapanda kwenda huko, akampiga Yoabu na kumuua, akazikwa nyumbani kwake nyikani.
-