5 Wakati huo, Adoniya+ mwana wa Hagithi alikuwa akijikweza, akisema: “Nitakuwa mfalme!” Alijitengenezea gari, naye akawa na wapanda farasi na wanaume 50 waliokimbia mbele yake.+
11 Ndipo Nathani+ akamuuliza Bath-sheba,+ mama ya Sulemani:+ “Je, hujasikia kwamba Adoniya+ mwana wa Hagithi amekuwa mfalme, na bwana wetu Daudi hajui lolote kuhusu jambo hilo?
24 Na sasa, kwa hakika kama Yehova anavyoishi, ambaye ameniimarisha kabisa+ na kuniketisha kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu na kunijengea nyumba* kama alivyoahidi,+ Adoniya atauawa+ leo.”