Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 5:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Hupaswi kamwe kuwa na miungu mingine ila mimi.*+

      8 “‘Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa+ au mfano wa* kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani au kilicho ndani ya maji chini ya dunia. 9 Usiviinamie wala kushawishiwa kuviabudu,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu ninayetaka watu waniabudu mimi peke yangu,+ nami huwaadhibu watoto kwa sababu ya makosa ya baba zao, kufikia kizazi cha tatu na kizazi cha nne cha wale wanaonichukia,+

  • Waamuzi 2:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini walikataa kuwasikiliza hata waamuzi hao, nao walifanya ukahaba na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia ambayo mababu zao walifuata, ambao walitii amri za Yehova.+ Walikataa kutii.

  • Waamuzi 8:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Mara tu baada ya Gideoni kufa, Waisraeli wakaanza tena kufanya ukahaba wa kiroho na Mabaali,+ nao wakamfanya Baal-berithi kuwa mungu wao.+

  • 2 Wafalme 17:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 nao walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu mahali pote pa juu kama yalivyofanya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kutoka mbele yao.+ Waliendelea kutenda maovu na kumkasirisha Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki