Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 31:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Iweni jasiri na imara.+ Msiogope wala msiwe na hofu mbele yao,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu ndiye anayepiga mwendo pamoja nanyi. Hatawatupa wala kuwaacha.”+

  • Kumbukumbu la Torati 31:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Yehova ndiye anayepiga mwendo mbele yako, naye ataendelea kuwa pamoja nawe.+ Hatakutupa wala kukuacha. Usiogope wala usihofu.”+

  • Yoshua 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia mababu zao kwamba nitawapa.+

  • Yoshua 1:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Je, si mimi niliyekuamuru uwe jasiri na imara? Basi uwe jasiri na imara. Usitetemeke wala kuogopa, kwa maana mimi Yehova Mungu wako nipo pamoja nawe mahali popote utakapoenda.”+

  • 2 Wafalme 6:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini Elisha akamwambia: “Usiogope!+ Kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”+ 17 Ndipo Elisha akaanza kusali na kusema: “Ee Yehova, tafadhali, mfungue macho yake, ili aone.”+ Mara moja Yehova akamfungua macho mtumishi huyo naye akaona, na tazama! eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita ya moto+ kumzunguka Elisha pande zote.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 20:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Akasema: “Sikilizeni kwa makini, enyi watu wote wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalemu na Mfalme Yehoshafati! Yehova anawaambia hivi: ‘Msiogope wala msihofu kwa sababu ya umati huu mkubwa, kwa maana vita si vyenu bali ni vya Mungu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki