Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 19:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Akajibu: “Nimekuwa na bidii kwelikweli kwa ajili ya Yehova Mungu wa majeshi;+ kwa maana Waisraeli wameliacha agano lako,+ wamebomoa madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga,+ nimebaki mimi peke yangu. Sasa wanataka kuniua.”*+

  • Zaburi 119:139
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 139 Bidii yangu inanila,+

      Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako.

  • Mathayo 21:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yesu akaingia hekaluni na kuwafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.+ 13 Akawaambia: “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’+ lakini ninyi mnaifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+

  • Marko 11:15-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Wakafika Yerusalemu. Akaingia hekaluni akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, naye akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,+ 16 na hakumruhusu mtu yeyote apite hekaluni akiwa amebeba chombo. 17 Alikuwa akiwafundisha akisema: “Je, haikuandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote’?+ Lakini mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+

  • Yohana 2:13-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, basi Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 14 Alipoingia hekaluni akakuta watu wakiuza ng’ombe, kondoo, na njiwa,+ pia, wale waliobadili pesa walikuwa kwenye viti vyao. 15 Basi akatengeneza mjeledi wa kamba na kuwafukuza hekaluni wote waliokuwa na kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za wale waliobadili pesa na kupindua meza zao.+ 16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”*+ 17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki