-
Marko 11:15-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Wakafika Yerusalemu. Akaingia hekaluni akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, naye akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,+ 16 na hakumruhusu mtu yeyote apite hekaluni akiwa amebeba chombo. 17 Alikuwa akiwafundisha akisema: “Je, haikuandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote’?+ Lakini mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+
-
-
Yohana 2:13-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, basi Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 14 Alipoingia hekaluni akakuta watu wakiuza ng’ombe, kondoo, na njiwa,+ pia, wale waliobadili pesa walikuwa kwenye viti vyao. 15 Basi akatengeneza mjeledi wa kamba na kuwafukuza hekaluni wote waliokuwa na kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za wale waliobadili pesa na kupindua meza zao.+ 16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”*+ 17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+
-