Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Au je, Mungu amewahi kujaribu kujichukulia taifa kutoka kati ya taifa lingine kwa hukumu,* kwa ishara, kwa miujiza,+ kwa vita,+ kwa mkono wenye nguvu,+ kwa mkono ulionyooshwa, na kwa matendo ya kutisha,+ kama Yehova Mungu wenu alivyowafanyia kule Misri mbele ya macho yenu wenyewe?

  • Nehemia 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kisha ukafanya ishara na miujiza dhidi ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua waliwatendea kwa kimbelembele.+ Ukajijengea jina ambalo limedumu hadi leo hii.+

  • Zaburi 105:27-36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Walifanya ishara zake kati yao,

      Miujiza yake katika nchi ya Hamu.+

      28 Alilituma giza na nchi ikawa giza;+

      Hawakuasi maneno yake.

      29 Alibadili maji yao yakawa damu

      Na kuwaua samaki wao.+

      30 Nchi yao ikajaa vyura,+

      Hata katika vyumba vya mfalme.

      31 Aliagiza nzi wavamie

      Na mbu* katika maeneo yao yote.+

      32 Aliibadili mvua yao ikawa mvua ya mawe

      Naye akatuma radi* katika nchi yao.+

      33 Aliipiga mizabibu yao na mitini yao

      Na kuivunjavunja miti ya eneo lao.

      34 Aliagiza nzige wavamie,

      Nzige wachanga wasio na idadi.+

      35 Walikula kabisa mimea yote nchini,

      Nao wakala kabisa mazao ya ardhi.

      36 Kisha akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+

      Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki