Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 11:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha Daudi akawatuma wajumbe wamlete.+ Basi akaja kwa Daudi, naye Daudi akalala naye.+ (Wakati huo mwanamke huyo alikuwa akijitakasa uchafu wake.*)+ Kisha, mwanamke huyo akarudi nyumbani kwake.

  • 2 Samweli 12:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako,+ kwa sababu ulinidharau kwa kumchukua mke wa Uria Mhiti awe mke wako.’ 11 Yehova anasema hivi: ‘Tazama, ninakuletea msiba kutoka katika nyumba yako mwenyewe;+ na mbele ya macho yako mwenyewe, nami nitawachukua wake zako na kumpa mwanamume mwingine,+ naye atalala na wake zako kweupe kabisa wakati wa mchana.*+

  • Methali 6:32-35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Mtu yeyote anayefanya uzinzi na mwanamke hana busara;*

      Yule anayefanya hivyo anajiangamiza mwenyewe.+

      33 Atapata tu majeraha na kuvunjiwa heshima,+

      Na aibu yake haitafutiliwa mbali.+

      34 Kwa maana wivu humfanya mume awake hasira;

      Hataonyesha huruma anapolipiza kisasi.+

      35 Hatakubali fidia* yoyote;

      Hutamtuliza, hata ukimpa zawadi kubwa kadiri gani.

  • Waebrania 13:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kisiwe na unajisi,+ kwa maana Mungu atawahukumu waasherati* na wazinzi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki