-
Hesabu 25:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Lakini wakati huo, Mwisraeli fulani akamleta mwanamke Mmidiani+ karibu na ndugu zake Waisraeli huku Musa na Waisraeli wote wakitazama walipokuwa wakilia kwenye mlango wa hema la mkutano. 7 Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa kuhani Haruni alipoona jambo hilo, aliinuka mara moja kutoka kati ya Waisraeli waliokusanyika, akachukua mkuki. 8 Kisha akamfuata mwanamume huyo Mwisraeli mpaka hemani, akawachoma mkuki wote wawili, nao ukapenya kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke huyo. Ndipo pigo lililowapata Waisraeli likakomeshwa.+
-
-
1 Samweli 15:22, 23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Ndipo Samweli akasema: “Je, Yehova hupendezwa zaidi na dhabihu za kuteketezwa na dhabihu nyinginezo+ kuliko kuitii sauti ya Yehova? Tazama! Kutii ni bora kuliko dhabihu,+ na kusikiliza kuliko mafuta+ ya kondoo dume; 23 kwa maana uasi+ ni sawa na dhambi ya uaguzi,*+ na kutenda kwa kimbelembele ni sawa na kutumia nguvu za uchawi na ibada ya sanamu.* Kwa kuwa umelikataa neno la Yehova,+ yeye pia amekukataa usiwe mfalme.”+
-